TAARIFA KWA UMMA
Posted on: September 2nd, 2021
Zoezi la utoaji chanjo linaendela katika kituo cha Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha Mount Meru, kila siku.
Wananchi walio tayari kuchanja wanapaswa kujisajili taarifa zao kupitia: chanjocovid.moh.go.tz, na kufika kituoni kwa ajili ya kuchanja.
Aidha, Vyeti vya Kielektroniki vimeanza kutolewa na yeyote ambaye amepata Chanjo ya UVIKO-19 anapaswa kurudi katika Kituo alipopatia Chanjo kusajiliwa taarifa zake na kupatiwa cheti hicho.