Uhasibu na Fedha

KITENGO CHA UHASIBU

Majukumu ya kitengo cha Fedha na Uhasibu yamegawanyika kwenye nyanja zifuatazo:

Kuwezesha Malipo:

  • Kuandaa na kuingiza malipo kwenye mtandao wa malipo
  • Kuchukua hundi zamalipo kutoka Hazina ndogo
  • Kupeleka fedha tasilimu na hundi benki
  • Kutayarisha taarifa za mwezi za malipo
  • Kuwalipa watumishi fedha taslimu au hundi na kuwalipa watoa huduma kwa hundi
  • Kutunza daftari la hesabu

Hesabu za Mwisho wa Mwaka:

  • Kutayarisha Makadirio ya bajeti na kudhibiti matumizi
  • Kuandaa taarifa ya matumizi ya robo mwaka, nusu mwaka na mwaka mzima kwa ajili ya kuiwasilisha kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali
  • Kujibu hoja zote na maoni ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
  • Kuandaa taarifa ya hesabu za mwisho wa mwaka na kuziwasilisha kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Ukusanyaji Mapato:

  • Kukusanya Mapato
  • Kusimamia mapato kwa mujibu wa sheria na miongozo

Ukaguzi wa Awali:

  • Kuhakiki nyaraka za malipo kama zimezingatia taratibu za malipo ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa
  • Kuhakikisha kama sheria, kanuni na miongozo na nyaraka za fedha kama zimezingatiwa
  • Kuhakikisha malipo yatakayofanyika hayavuki bajeti ya kasma husika